Pata taarifa kuu
TUNISiA-SIASA

Tunisia: Rais aahidi kuteua serikali na kufanyia marekebisho Katiba

Baada ya hali ya hatari kutangazwa Julai 25, rais wa Tunisia Kaïs Saïed, hatimae, anataka kufanyia marekebisho Katiba ya 2014. Hivi ndivyo alisema, Jumamosi jioni Septemba 11, akitangaza, wakati huo huo, kuundwa kwa serikali hivi karibuni.

Rais wa Tunisia Kaïs Saïed.
Rais wa Tunisia Kaïs Saïed. MOHAMED KHALIL / AFP
Matangazo ya kibiashara

Akiongea na wafuasi wake na vyombo vichache vya habari, Kaïs Saïed aliweka wazi nia yake. Alizungumzia kuhusu marekebisho ya Katiba.

“Lazima tufanye mabadiliko katika mfumo wa Katiba. Katiba sio za milele, zinaweza kubadilishwa! Mabadiliko yanapaswa kuwafaa raia wa Tunisia, kwa sababu baada ya yote, mamlaka ni yao, ”alisema. Na ili marekebisho yake ya katiba yapitishwe, Kaïs Saïed kwa hivyo alisema atatumia kura ya maoni.

Mkuu wa Nchi pia yuko mbioni kutangaza serikali mpya: "Ninawahakikishia kwamba watu watakaoteuliwa watakuwa waaminifu, ambao hawatokwenda kinyume na ahadi zao," alisema. Wiki saba zilizopita, Bwana Saïed alichukua madaraka yote ya kiutendaji na kusitisha shughuli za bunge.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.