Pata taarifa kuu
UN - UBAGUZI WA RANGI

UN -Tatua swala la ubaguzi wa rangi duniani

Umoja wa mataifa umezitaka serikali kote  duniani kumheshimu mmarekani mweusi George Floyd, aliyeuawa na polisi mzungu Derek Chauvin, mwaka uliopita nchini Marekani, kwa kutatua swala la ubaguzi wa rangi, katika mataifa yao.

 Michelle Bachelet mkuu wa UN kuhusu haki za binadamu.
Michelle Bachelet mkuu wa UN kuhusu haki za binadamu. CRISTIAN HERNANDEZ / AFP
Matangazo ya kibiashara

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa ripoti ya mauwaji ya Floyd, mkuu wa haki za binadamu wa umoja wa mataifa, Michelle Bachelet, amesema njia pekee ya kumheshimu Floyd ni serikali katika mataifa yote duniani kutatua swala la ubaguzi wa rangi analosema linarejesha nyuma hatua zilizopingwa kwa dunia kuendelea.

Ripoti hiyo inaeleza kuwa hali ya ubaguzi wa rangi duniani ni ya kutisha, na kwamba raia wengi wenye asili ya Kiafrica, hupitia mateso mikoni mwa maafisa wa usalama kote duniani.

Ripoti hiyo inasema raia wenye asili ya kiafrica hubaguliwa wakati wanapotafuta, ajira, nyumba na masomo na kushtumu serikali kwa kukosa kuangazia kwa kina swala hilo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.