Watu 10 watekwa nyara Beni, DRC
Watu waliokuwa wamejihami kwa silaha wameripotiwa kuwateka nyara watu zaidi ya 10 kwenye mji wa Beni mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Imechapishwa:
Miongoni mwa waliotekwa ni mkurugenzi wa radio washirika wa RFI, RTGB Beni ambayo huwa inajiunga na matangazo yetu ya Kiswahili.
Mashuhuda wanasema watu hao walikuwa wamevalia sare za kijeshi ambapo baadae walitokemea na mateka wao kusikojulikana baada ya kuwapora kila walichokuwa nacho.
Makundi ya waasi wakiwemo Mai-Mai na kundi la ADF yamekuwa yakiyumbisha usalama kila uchao katika maeneo hayo kiasi kwamba hadi sasa ni vigumu kubaini wahusika.
kundi la waasi wa Uganda linaloendesha harakati zake mashariki mwa DRC, limewaua mami ya watu katika maeneo mmbalimbali jirani na mji wa Beni.
Hivi karibuni jeshi la Uganda (UDF) likishirikiana na jeshi la DRC, (FARDC) liliendesha operesheni kabambe mashariki mwa DRC dhidi ya kundi hili.