Pata taarifa kuu
SIMBA SC-MBABANE SWALLOWS-KLABU BINGWA AFRIKA

Simba SC, Gor Mahia, Vipers na APR zafahamu wapinzani wao, michuano ya Klabu bingwa Afrika

Ratiba ya Michuano ya klabu bingwa Afrika imetangazwa leo huku ikionyesha mabingwa wa soka Tanzania Simba SC kuwa watachuana na Mabingwa wa Eswatin, Mbabane Swallows.

Ratiba ya Michuano ya klabu Afrika
Ratiba ya Michuano ya klabu Afrika CAF
Matangazo ya kibiashara

Kwa mujibu wa ratiba hiyo, Mchezo wa kwanza baina ya Simba na Mbabane Swallows utachezwa ama tarehe 27 au 28 mwezi huu Jijini Dar es Salaam kabla ya kurudiana wiki moja baadaye Mjini Mbabane.

Mshindi baina ya Simba na Mbababe atachuana nan mshindi baina ya Nkana ya Zambia na Uniao Desportiva Do Songo ya Msumbiji.

Mechi nyingine za awali ni kama ifuatavyo

Gor Mahia ya Kenya itachuana na Big Bullets ya Malawi

Asas Djibout Telecom ya Djibout itakumbana na Jima Abijafar ya Ethiopia

Orlando Piratees ya Afrika Kusini itakumbana na Light Star ya Ushelisheli

Le Messenger Ngozi ya Burundi itakuwa mwenyeji wa Ismailia ya Misri

AS Sonidep ya Niger itakuwa mwenyeji wa Zesco ya Zambia

ASFB ya Burkinafaso itakuwa mwenyeji wa Coton Sports ya Cameroon

APR ya Rwanda itakumbana na Club Africaine ya Tunisia

Al Hilal ya Sudan itacheza na JKU ya Zanzibar

Vipers ya Uganda itaanzia ugenini kwa kuchuana na El Merreikh ya Sudan

Katika Kombe la Shirikisho baadhi za awali zitakuwa kama ifuatavyo

Zimamoto ya Zanzibar itachuana na Kazier Chiefs ya Afrika Kusini

DC Motema Pembe itachuana na Les Anges De Fatima

AS Nyuki itaanzia ugenini dhidi ya Al Ahly Shandi ya Sudan

Mtibwa Sugar ya Tanzania itachuana na Nothern Dynamo ya Ushelisheli

Gambia Armed Forces itakumbana na San Pedro

Petro Atletico ya Angola itakuwa mwenyeji wa Orapa United ya Botswana

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.