Pata taarifa kuu

Emmanuel Macron ziarani Prague: 'Lazima tuwe na ufahamu juu ya ukweli wa hali ya mambo'

Rais wa Ufarasa Emmanuel Macron yuko ziarani siku ya Jumanne, Machi 5 nchini Jamhuri ya Czech. Safari iliyozinduliwa kwa kiasi kikubwa na suala la Ukraine. Baada ya kuongeza uwezekano wa kutuma wanajeshi wa nchi za Magharibi, rais wa Ufaransa ametoa wito kwa washirika wa Ukraine "kutokuwa waoga" mbele ya Urusi ambayo imekuwa, "isiyozuilika" amesema rais wa Ufransa.

Rais wa Jamhuri ya Czech Petr Pavel na mwenzake wa Ufaransa Emmanuel Macron wakikagua Gwaride la Heshima lililoandaliwa na Jeshi la Ulinzi wakati wa hafla ya kuwakaribisha kwenye Jumba la Prague, Jumanne hii Machi 5, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Czech Petr Pavel na mwenzake wa Ufaransa Emmanuel Macron wakikagua Gwaride la Heshima lililoandaliwa na Jeshi la Ulinzi wakati wa hafla ya kuwakaribisha kwenye Jumba la Prague, Jumanne hii Machi 5, 2024. AFP - MICHAL CIZEK
Matangazo ya kibiashara

Na mwandishi wetu maalum huko Prague, Charlotte Urien-Tomaka

Katika hotuba yake kwa jumuiya ya Wafaransa wishio nchini Jamhuri ya Czech, Emmanuel Macron ameonyesha msimamo wa nchi yake: "Kwa hakika tunakaribia wakati katika Ulaya yetu ambapo itakuwa sahihi kutokuwa waoga. Hatutaki kamwe kuona majanga yanayokuja. Hatutaki kamwe kuona kinachoendelea. Na tutalazimika kuishi kulingana na Historia, na ujasiri unaomaanisha. "

Vita nchini Ukraine hatimaye viliibuka kama mada kuu ya ziara hii, hadi kufikia hatua ya kufidia kutiwa saini kwa mkataba wa mabilioni ya dola na EDF, na kusakinishwa kwa vinu vinne vya nyuklia na kampuni ya Ufaransa.

Baadaye mchana, wakati wa mkutano na waandishi wa habari na mwenzake wa Jamhuri ya Czech Petr Pavel, Emmanuel Macron alirejelea maoni yake yaliyokosolewa juu ya kutuma wanajeshi nchini Ukraine, akionekana kuyakubali: "Ni hatua ya kimkakati ambayo niliita na ninachukua jukumu kikamilifu. Ni lazima tuwe waangalifu kuhusu hali halisi ya mambo ilivyo barani Ulaya. "

Rais wa Ufaransa ameweka wazi anachofikiria: "Nimesema mfumo ni upi. Sikusema kulikuwa na makubaliano. Lakini nadhani ilikuwa muhimu kuifanya kwa sababu sote tunahitaji kufahamu. Kwa upande wake, ikiwa Petr Pavel ametoa msaada wake kwa mkuu wa nchi, akisema "yuko wazi kwa idadi nzima ya uwezekano", hakutaka kujitolea kwa wazo la kutuma askari wa ardhini nchini Ukraine.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.