Pata taarifa kuu

Urusi yatekeleza mashambulio makubwa nchini Ukraine

Jeshi la Urusi limeishambulia Ukraine kwa kurusha makombora  122 na kutumia ndege zisizo na rubani 36 kurusha mabomu katika maeneo mbalimbali  na kusababisha vifo vya watu 18.

Mashambulio ya jeshi la Urusi nchini Ukraine
Mashambulio ya jeshi la Urusi nchini Ukraine REUTERS - GLEB GARANICH
Matangazo ya kibiashara

Mashambulio ya Ijumaa, yameelezwa kuwa makubwa zaidi kuwahi kushuhudiwa katika vita kati ya nchi hizo mbili, ambavyo vimedumu kwa miezi 22 sasa.

Jiji la Kiev limeshuhudia mashambulio yenye nguvu, na kuacha moshi mzito mweusi angani, katika maeneo yaliyoshambuliwa na jeshi la Urusi.

Mbali na Kiev, miongoni mwa miji mingine sita  iliyoshambuliwa ni pamoja na Lviv , Odesa na Zaporizhzhia Kusini huku majengo yakiangushwa zikiwemo hospitali.

Hatua hii ya Urusi imekuja baada ya mapema wiki hii, jeshi la Ukraine kushambulia na kuharibu manuari ya kivita ya Urusi kwenye bandari ya Bahari nyeusi kwenye jimbo  la Crimea.

Umoja wa Mataifa, Umoja wa Ulaya na nchi za Magharibi zikiongozwa na Ufaransa yamelaani hatua hiyo ya Urusi, huku rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky, akisema nchi yake imeshambuliwa na vifaa karibu vyote ya kivita.

Aidha, Zelensky ameyataka mataifa ya Magharibi kuendelea kuiunga mkono kwa kuipa fedha na vifaa vya kijeshi, baada ya Marekani wiki hii kutoa msaada wake wa kifedha wiki hii.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.