Pata taarifa kuu

Wahamiaji wanne wamezama nchini Ugiriki

Wahamiaji wanne wameuwa katika ajali ya boti katika visiwa vya Lesbos nchini Ugiriki wengine 18 wakiwa wameokolewa.

Wahamiaji waliookolewa wakishuka kwenye meli ya Hellenic Coast Guard kwenye bandari ya Mytilene, kufuatia ajali ya meli ambapo wahamiaji wanne walikufa maji, nje ya kisiwa cha Lesbos, Ugiriki, Agosti 28, 2023. REUTERS/Elias Marcou
Wahamiaji waliookolewa wakishuka kwenye meli ya Hellenic Coast Guard kwenye bandari ya Mytilene, kufuatia ajali ya meli ambapo wahamiaji wanne walikufa maji, nje ya kisiwa cha Lesbos, Ugiriki, Agosti 28, 2023. REUTERS/Elias Marcou REUTERS - ELIAS MARCOU
Matangazo ya kibiashara

Waliookolewa walipelekwa katika eneo la Mytilene, mji mkuu wa Lesbos, eneo kuu ambalo wahamiaji hutumia wakitokea nchini Uturuki.

Hakuna taarifa iliyotolewa kuhusu uraia wa wahamiaji hao na hali ya kiafya ya waliookolewa.

Mwezi Juni, boti ya uvuvi iliyokuwa imejaa wahamiaji zaidi ya 750 wakitokea nchini Libya ilizama ikielekea nchini Ugiriki.

Wahamiaji waliookolewa wakishuka kwenye meli ya Hellenic Coast Guard kwenye bandari ya Mytilene, kufuatia ajali ya meli ambapo wahamiaji wanne walikufa maji, nje ya kisiwa cha Lesbos, Ugiriki, Agosti 28, 2023. REUTERS/Elias Marcou
Wahamiaji waliookolewa wakishuka kwenye meli ya Hellenic Coast Guard kwenye bandari ya Mytilene, kufuatia ajali ya meli ambapo wahamiaji wanne walikufa maji, nje ya kisiwa cha Lesbos, Ugiriki, Agosti 28, 2023. REUTERS/Elias Marcou REUTERS - ELIAS MARCOU

Karibia wahamiaji 100 waliookolewa na ilidaiwa kuwa wengine 600 walizama kwa mujibu wa takwimu kutoka Ugiriki.

Maelfu ya wahamiaji wengi wakitokea nchini Syria, Afghanistan na Pakistan, wameripotiwa kuingia nchini Ugiriki wakitumia bahari na maeneo ya mpaka na Uturuki.

Kutokana na sheria kali kuhusu uhamiaji, Ugiriki imeimarisha uchunguzi katika bahari kwenye mpaka wake na Uturuki.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.