Pata taarifa kuu

Watu 33 wamefariki katika mlipuko nchini Urusi

Nairobi – Takriban watu 33 wameuwa katika mlipuko kwenye kituo cha petroli katika jimbo linalojitawala la Dagestan nchini Urusi, wizara ya afya imethibitisha.

Watu 33 wamethibitishwa kufariki katika tukio hilo
Watu 33 wamethibitishwa kufariki katika tukio hilo AP
Matangazo ya kibiashara

Watu 80 wameripotiwa kujeruhiwa wakiwemo watoto watatu kwenye mlipuko huo katika mji wa Makhachkala. Rais Putin ametuma pole zake kwa waathirwa wa mkasa huo.

Picha zilizosambazwa na wizara ya masuala ya dharura nchini humo zimeonyesha magari yalioharibiwa vibaya katika mlipuko huo wakati maofisa wa uokozi wakijaribu kuzima moto mkubwa katika eneo la tukio.

Mamlaka inasema imeanzisha uchunguzi kubaini chanzo cha moto huo
Mamlaka inasema imeanzisha uchunguzi kubaini chanzo cha moto huo AP

Serikali imsema watu 30 walifariki katika mkasa huo wakati wengine 80 wakiwa wakiachwa na majeraha.

Mlipuko huo umetokea katika mji wa Makhachkala baada ya moto kutokea katika kituo kimoja cha petrol.

Rais wa Urusi ametuma pole zake kwa waathiriwa wa mkasa huo
Rais wa Urusi ametuma pole zake kwa waathiriwa wa mkasa huo AP

Mamlaka imesema mlipuko huo pia umeharibu majengo na magari mengine yaliokuwa karibu na eneo la tukio. Tayari uchunguzi umeanzishwa kubaini chanzo cha moto huo.

Serikali ya Dagestan imetangaza siku ya Agosti 15 kuwa siku ya maombolezo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.