Pata taarifa kuu
USHIRIKIANO-DIPLOMASIA

Ukraine: Zelensky na Lula washindwa kukutana kwa mazungumzo Hiroshima

Mkutano kati ya Rais wa Ukraine Zelensky na mwenzake wa Brazil Lula haukufanyika huko Hiroshima, nchini Japan. Rais wa Brazil Lula da Silva anasema alimsubiri mwenzake wa Ukraine kando ya mkutano wa nchi zilizostawi zaidi kiviwanda, G7, lakini hakuja.

Rais wa Brazil Luiz Inacio Lula da Silva (c) akiwa na Waziri Mkuu wa Vietnam Pham Minh Chinh, Waziri Mkuu wa Japan Fumio Kishida, Katibu Mkuu wa OECD Mathias Cormann na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres, wakati wa mkutano wa kilele wa G7 huko Hiroshima, Japan, Mei 21. , 2023.
Rais wa Brazil Luiz Inacio Lula da Silva (c) akiwa na Waziri Mkuu wa Vietnam Pham Minh Chinh, Waziri Mkuu wa Japan Fumio Kishida, Katibu Mkuu wa OECD Mathias Cormann na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres, wakati wa mkutano wa kilele wa G7 huko Hiroshima, Japan, Mei 21. , 2023. via REUTERS - POOL
Matangazo ya kibiashara

Na mwandishi wetu huko São Paulo, Martin Bernard 

Rais wa Ukraine alichukua fursa ya safari yake ya Japan kukutana na viongozi wengi, akiwemo Waziri Mkuu wa India Narendra Modi, ambaye alikataa kulaani uvamizi wa Urusi nchini Ukraine.

Msimamo wa Brazil ni tofauti: Lula anatambua kuwa Moscow ni mchokozi, lakini anataka kumaliza vita kwa njia ya mazungumzo, na sio kwa kuzidisha mzozo - wakati G7 ndiyo kwanza imejitokeza kuunga mkono mauzo mapya ya silaha kwa Ukraine.

Tukio hili la wawili hao kushindwa kukutana hukoHiroshima linakuja wiki moja baada ya mshauri wa kidiplomasia wa Lula kusafiri kwenda Kyiv. Celso Amorim kisha akaelezea msimamo wa Brazil… Baada ya ziara ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi huko Brasilia, Sergei Lavrov, mwezi uliopita.

Baada ya mkutano wa G7, mpango wa Lula kuunda "klabu ya amani" kwa Ukraine bado unaonekana kukwama.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.