Pata taarifa kuu

NATO: Nchi wanachama zitaendelea kushirikiana na Japan

Katibu mkuu wa Jumuiya ya Kujihami ya nchi za Magharibi, NATO, Jens Stoltenberg, amesema nchi wanachama zitaendelea kushirikiana na Japan, hasa wakati huu ambao usalama wan chi zao unatishiwa na uvamizi wa Urusi nchini Ukraine.

Katibu mkuu wa NATO Jens Stoltenberg na waziri mkuu wa Japan Fumio Kishida
Katibu mkuu wa NATO Jens Stoltenberg na waziri mkuu wa Japan Fumio Kishida via REUTERS - POOL
Matangazo ya kibiashara

Stoltenberg, amesema ziara yake kwenye miji ya Tokyo na Seuol, Korea Kusini, inalenga kuimarisha ushirikiano wa kijeshi baina ya nchi hizo, na kwamba watahakikisha dunia inaendelea kuwa salama.

“Vita nchini Ukraine vinatuonyesha kuwa usalama wetu kwa pamoja unategemeana.”ameeleza Jens Stoltenberg.

Mataifa wanachama wa NATO wamekuwa wakitoa wito wa kushirikiana ilikupambana na kile wanachosema ni tishio la dunia kutoka kwa mataifa kama Urusi na Korea kaskazini.

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.