Pata taarifa kuu

Washirika wa NATO kuipatia Ukraine silaha 'nzito na za kisasa zaidi'

Washirika wa NATO wataipatia Ukraine silaha 'nzito na za kisasa zaidi' ili kuisaidia kukabiliana na mashambulizi ya Urusi, Katibu Mkuu wa NATO Jens Stoltenberg ametangaza siku ya Jumatano.

Andrzej Duda, Rais wa Poland, kushoto, akihutubia kikao akiwa karibu na Jens Stoltenberg, Katibu Mkuu wa NATO, wakati wa mkutano wa 53 wa kila mwaka wa Jukwaa la Uchumi Duniani, WEF, huko Davos, Uswisi, Jumatano, tarehe 18, 2023. Mkutano huo unawaleta pamoja wafanyabiashara, wanasayansi, viongozi wa mashirika na wa vyama kisiasa huko Davos chini ya mada "Ushirikiano katika Ulimwengu uliogawanyika" kuanzia Januari 16 hadi 20.
Andrzej Duda, Rais wa Poland, kushoto, akihutubia kikao akiwa karibu na Jens Stoltenberg, Katibu Mkuu wa NATO, wakati wa mkutano wa 53 wa kila mwaka wa Jukwaa la Uchumi Duniani, WEF, huko Davos, Uswisi, Jumatano, tarehe 18, 2023. Mkutano huo unawaleta pamoja wafanyabiashara, wanasayansi, viongozi wa mashirika na wa vyama kisiasa huko Davos chini ya mada "Ushirikiano katika Ulimwengu uliogawanyika" kuanzia Januari 16 hadi 20. © AP / Gian Ehrenzeller
Matangazo ya kibiashara

"Tutakutana (Ijumaa) huko Ramstein (Ujerumani) katika kikundi cha mawasiliano cha Ukraine kinachoongozwa na marekani na ujumbe mkuu itakuwa kuongezwa msaada kwa silaha nzito na za kisasa zaidi," amesema, akiwa nchini Uswisi.

wakati huo huo watu watatu wakuu katika wizara ya mambo ya ndani ya Ukraine wameuawa katika ajali ya helikopta kando ya kitalu katika kitongoji cha mashariki mwa mji mkuu Kyiv.

Waziri wa Mambo ya Ndani Denys Monastyrsky, 42, alikufa pamoja na naibu wake wa kwanza wa waziri na katibu wa serikali.

Watu 16 walikufa wakati helikopta hiyo ilipoanguka huko Brovary, wakiwemo watoto watatu, kulingana na maelezo yaliyosasishwa kutoka kwa rais wa Ukraine.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.