Pata taarifa kuu

Volodymyr Zelensky apuuzia mbali wito wa kusitisha vita wa Urusi

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky, amepuuzia wito wa mwenzake wa Urusi Vladimir Putin, ambaye ametangaza usitishwaji wa vita, wakati dhehebu la Orthodox  linapoadhimisha sikukuu ya Krismasi.

Volodymyr Zelensky, wakati wa hotuba yake kwa Bunge la Marekani, Desemba 21, 2022 huko Washington.
Volodymyr Zelensky, wakati wa hotuba yake kwa Bunge la Marekani, Desemba 21, 2022 huko Washington. © AP/Carolyn Kaster
Matangazo ya kibiashara

Rais Zelenskyy, amesema tangazo la Putin, ni mbinu ya kurudisha nyuma jitihada za jeshi la Ukraine, kuendelea kulikomboa jimbo la Donbasa, Mashariki mwa nchi yake na Urusi inataka kutumia fursa hiyo kuwaingiza zaidi wanajeshi wake nchini Ukraine. 

Aidha, Ukraine inasema vita vitaisha iwapo Urusi itaondoa wanajeshi wake, katika ardhi yake. Naye Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guteress amesema anakaribisha usitishwaji wowote wa kusitisha vita, katika sikukuu ya Krismasi, licha ya kwamba  hatua hiyo haiwezi kumaliza vita vinavyoendelea. 

Siku ya Alhamisi, rais Putin alitangaza kuwa jeshi lake halitaendeleza vita kwa saa 36, kuanzia saa tatu asubuhi, saa za Kimataifa mpaka siku ya Jumamos saa tatu usiku, ili kutoa nafasi kwa waumini wa dhehebu la Orthodox  nchini Urusi kusherehekea krismasi siku ya Jumamosi. 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.