Mvutano wa kisiasa waendelea kuikumba Italia
Waziri mkuu wa Italia ameendelea kuliunganisha pamoja baraza la mawaziri nchini humo licha ya kukataliwa na mwanasiasa mashuhuri zaidi ambaye jitihada zake kushika madaraka ziligonga mwamba.
Imechapishwa:
Carlo Cottarelli, mtaalamu wa uchumi wa zamani katika taasisi ya fedha ya kimataifa IMF alikataliwa na rais Sergio Mattarella, hatua iliyosababisha sauti za kulaani uamuzi wa rais.
Italia, mojawapo ya nchi yenye uchumi mkubwa katika Umoja wa Ulaya, imeingia katika mgogoro baada ya Rais Sergio Mattarella mwishoni mwa wiki kukataa uteuzi wa serikali ambao ulimpa uwaziri wa fedha mtaalamu wa zamani wa uchumi katika IFM.
Hatua hiyo imesababisha waziri mkuu wa nchi hiyo kujiuzulu ikimaanisha harakati za pande mbili kuunda serikali zikishindikana.