Pata taarifa kuu
ITALIA-UCHAGUZI-SIASA

Raia wa Italia wasubiri matokeo ya Uchaguzi wa wabunge

Matokeo ya awali kuhusu Uchaguzi wa Wabunge nchini Italia, yanaonesha kuwa hakuna chama kitachopata idadi kubwa ya viti vinavyohitajika ili kuunda serikali pekee yake.

Waziri Mkuu wa zamani  Silvio Berlusconi, akipiga kura Jumapili Machi 4 2018
Waziri Mkuu wa zamani Silvio Berlusconi, akipiga kura Jumapili Machi 4 2018 REUTERS/Stefano Rellandini
Matangazo ya kibiashara

Hata hivyo, hadi sasa muungano wa siasa unaoegemea mrengo wa kulia, unaongozwa na Waziri Mkuu wa zamani Silvio Berlusconi unatarajiwa kushinda.

Hata hivyo, ushindi huo unatarajiwa kuwa kati ya wabunge 225 au 265 kinyume na wabunge 316 kama inavyohitajika ili kuunda serikali.

Matokeo rasmi yanatarajiwa kufahamika baadaye siku ya Jumatatu.

Chama kitakachounda serikali, kitakuwa na kazi kubwa ya kuimarisha uchumi, kuunda nafasi za kazi na kupambana na wimbi la wakimbizi wanaokimbilia nchi hiyo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.