Pata taarifa kuu
UTURUKI-UJERUMANI

Uturuki yamuitisha balozi wake Ujerumani

Uturuki imemuitisha balaozi wake nchini Ujerumani kutokana na uamuzi wa Bunge la Ujerumani kupitisha Alhamisi hii azimio linalotambua mauaji ya kimbari ya Waarmenia.

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan (kushoto) na Kansela wa Ujrumani Angela Merkel Februari 4, 2014  Berlin.
Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan (kushoto) na Kansela wa Ujrumani Angela Merkel Februari 4, 2014 Berlin. AFP PHOTO / PATRIK STOLLARZ
Matangazo ya kibiashara

Ujerumani inabaini kwamba mauaji hayo yalitekelezwa na utawala wa Ottoman. Serikali ya Uturuki imefutilia mbali tuhuma hizo, Waziri Mkuu wa Uturuki, Binali Yildirim, ametangaza.

"Balozi wa Uturuki nchini Ujerumani ameitishwa kwa mashauriano," Bw Yildirim amesema, akinukuliwa na shirika la habari linalounga mkono serikali la ANATOLIA.

Kwa upande wake rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan amesema azimio la Bunge la Ujerumani litaathiri mahusiano ya Uturuki na Ujerumani.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.