Pata taarifa kuu
UHISPANIA-SIASA

Chama cha PSOE champitisha tena Rajoy kuwa Waziri Mkuu

Chama cha Kisoshalisti nchini Uhispania cha PSOE kwa kauli moja kimeidhinisha kuundwa kwa serikali ya kisoshalisti ya wachache, na hivyo kumaliza hali ya mfululizo wa mdororo wa kisiasa uliyodumu miezi kumi katika chaguzi mbili za wabunge zilizopita bila kuwa na idadi kubwa inayohitajika.

Mariano Rajoy, ambaye chama chake kilishinda chaguzi mbili za wabunge zilizopita bila kuwa na idadi kubwa inayohitajika, wameshindwa kuunda serikali ya umoja.
Mariano Rajoy, ambaye chama chake kilishinda chaguzi mbili za wabunge zilizopita bila kuwa na idadi kubwa inayohitajika, wameshindwa kuunda serikali ya umoja. REUTERS/Juan Medina
Matangazo ya kibiashara

Chama cha Kisoshalisti kilikua kimeweka mbele chaguo la uchaguzi wa tatu wa wabunge katika siku za usoni au matarajio ya kuundwa serikali mpya inayoongozwa na Mariano Rajoy.

Viongozi wa chama cha Kisoshalisti wameamua baada ya mkutano maalum mapema Jumapili mchana, kujizuia katika kura ya kuwa na imani ambayo Waziri Mkuu anayemaliza muda wake anatarajia kuwasilisha kwa Bunge wiki ijayo. Uamuzi huu wa kujizuia, ambao utamruhusu Mariano Rajoy kuanza muhula wa pili, ulipitishwa kwa kura 139 dhidi ya kura 96.

Akitetea matokeo haya, kiongozi wa mpito wa chama cha Kisoshalisti cha PSOE, Javier Fernandez, amesema kuwa uamuzi huo ulikua mbaya kidogo ikilinganishwa na maamuzi mawili.

"Tumejaribu kushinda uchaguzi, lakini kuona tu kwamba hilo halikufanyika, tunahitaji kuwa na serikali ili tuweze kuwa na wajibu wetu wa upinzani," Bwa Fermandez amesema.

Mariano Rajoy, ambaye chama chake kilishinda chaguzi mbili za wabunge zilizopita bila kuwa na idadi kubwa inayohitajika, wameshindwa kuunda serikali ya umoja.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.