Gabon yawasilisha malalamiko yake mbele ya ICC
Viongozi wa Gabon imemuomba Mwendesha Mashitaka mkuu kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) kuchunguza hali inayoendelea kushuhudiwa nchini humo.
Imechapishwa:
Mwendesha mashitaka Fatou Bensouda amesema kuwa ofisi yake itafanya mapitio ya mwanzo ya hali inayojiri ili kuamua kama vigezo vinavyohitajika kwa kufungua uchunguzi vimekamilika.
Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu ICC itatathmini taarifa zinazohusiana na uhalifu unaodaiwa kufanywa na kikundi chochote au mtu binafsi kushiriki katika hali hii.
Kisha mwendesha atatangaza dhidii ya ufunguzi wa uchunguzi.
ICC inaweza kutumia mamlaka yake katika heshima ya vitendo vya mauaji ya kimbari, uhalifu dhidi ya ubinadamu na uhalifu wa kivita uliofanywa katika mataifa yote yaliyotia saini Mkataba wa Roma, ikiwa ni pamoja Gabon.