Pata taarifa kuu
UINGEREZA-EU

Uingereza yapiga kura ya kujitoa katika Umoja wa Ulaya

Vyombo vya Habari nchini Uingereza vinatabiri kuwa, raia wa Uingereza wamepiga kura ya kujiondoa kwenye Umoja wa Ulaya.

Waingereza waamua kwa 52% ya kura Uingereza kuondaka katika EU, katika kura ya maoni iliyopigwa Alhamisi Juni 23, 2016.
Waingereza waamua kwa 52% ya kura Uingereza kuondaka katika EU, katika kura ya maoni iliyopigwa Alhamisi Juni 23, 2016. PHILIPPE HUGUEN / AFP
Matangazo ya kibiashara

Matokeo ya kura hiyo ya maoni iliyopigwa Alhamisi wiki hii, kuamua ikiwa nchi hiyo isalie au ijiondoe kwenye Umoja huo yanaendelea kutolewa na imetabiriwa kuwa waliopiga kura ya kujiondoa watashinda kwa asilimia 52 huku waliopiga ya kusalia katika Umoja huo wakipata asilimia 48.

Matokeo haya yamesababisha mtikisiko mkubwa kwenye soko la fedha duniani na pauni ya Uingereza imeshuka sana thamani kiwango ambacho mara ya mwisho kilishuhudiwa mwaka 1985.

Scotland na jiji la London, ripoti zinasema walipiga kura kwa wingi kusalia kwenye Umoja wa Ulaya.

Mmoja wa viongozi wa upinzani ambaye amekuwa katika mstari wa mbele kutaka Uingereza kujiondoa kwenye Umoja huo, Nigel Farage, amesema ushindi huu ni kama Uhuru kwa Uingereza.

Watu Milioni 30 walijitokeza kupiga kura, sawa na asilimia 71 nukta 8.
Wachambuzi wa uchumi duniani, wanasema ni siku ngumu sana kwa Uingereza kiuchumi lakini pia kwa Umoja wa Ulaya.

Inatarajiwa kuwa nchi hiyo itayumba kiuchumi baada ya uamuzi huu wa kuondoka kwenye Umoja wa Ulaya.

Picha iliyopigwa Desemba 15, 2011 katika mji wa kaskazini mwa Lille, inaonyesha noti za Euro 5, 10, 20 na 50.
Picha iliyopigwa Desemba 15, 2011 katika mji wa kaskazini mwa Lille, inaonyesha noti za Euro 5, 10, 20 na 50. AFP/ PHILIPPE HUGUEN

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.