Pata taarifa kuu

Mechi za AFCON: DR Congo na Zambia zafungua kwa sare

NAIROBI – Yoane Wissa aliifungia Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo bao la kusawazisha katika mechi yake ya kwanza dhidi ya Zambia iliyomalizika kwa sare ya 1-1, baada ya kupokea pasi ya uhakika kutoka kwa Cedric Bakambu.

Wachezaji wa timu ya taifa ya DRC
Wachezaji wa timu ya taifa ya DRC AP - Themba Hadebe
Matangazo ya kibiashara

Mechi hii ya kuwania taji la AFCON, ilichezwa Jumatano usiku kwenye mji wa Pwani wa San-Pedro. 

Zambia ndio iliyokuwa ya kwanza kupata bao katika dakika za mapema za mchuano huo, kupitia mchezaji wake Kings Kangwa, aliyemchenga kipa wa DRC Lionel Mpasi. 

Wachezaji wa timu ya taifa ya Zambia baada ya kupata bao dhidi ya DRC.
Wachezaji wa timu ya taifa ya Zambia baada ya kupata bao dhidi ya DRC. AP - Themba Hadebe

Sare ya nchi hizo jirani, ilikuja baada ya Morocco, kuipa Tanzania kipigo cha mabao 3-0 katika mechi ya kwanza ya kundi la F. 

Katika mchuano huo, Leopard ya DRC ilikuwa imepata penalti, lakini uamuzi huo ulibadilishwa na mwamuzi baada ya kubainika kuwa mchezaji Tandi Mwape hakuunawa mpira uliokuwa umepigwa na Arthur Masuaku. 

Kocha wa Zambia Avram Grant, amesema licha ya matokeo hayo kutokuwa ya kuridhisha, mabingwa hao wa mwaka 2012, wanatarajia kufanya vema katika mechi mbili zinazosalia kati ya Morocco na Tanzania. 

Zambia ilitoka sare ya moja kwa moja dhidi ya DRC
Zambia ilitoka sare ya moja kwa moja dhidi ya DRC AP - Themba Hadebe

Chipolopolo sasa itachuana na Taifa Stars siku ya Ijumaa, wakati vijana wa kocha Sebastien Desabre wakichuana na Atlas Lions ya Morocco. 

Ratiba ya leo, Januari 18 2024  

Equitorial Guinea V Guinea Bissau 

Cote d’Ivoire V Nigeria 

Misri V Ghana 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.