Pata taarifa kuu

Sahabo raia wa Rwanda kuondoka Lille ya Ufaransa

NAIROBI – Na Paulo Nzioki

Hakim Sahabo raia wa Rwanda amekuwa akiichezea klabu ya LOSC Lile ya nchini Ufaransa ya wachezaji wasiozidi umri wa miaka 19
Hakim Sahabo raia wa Rwanda amekuwa akiichezea klabu ya LOSC Lile ya nchini Ufaransa ya wachezaji wasiozidi umri wa miaka 19 © Hakim Sahabo facebook
Matangazo ya kibiashara

Mchezaji wa kimataifa wa Rwanda, Hakim Sahabo ameiaga klabu ya Ufaransa LOSC Lille akitajwa kuhamia Standard Liege ya Ubelgiji.

Standard Liege inayoshiriki katika ligi kuu nchini Ubelgiji Timu Jupiler Pro League inatajwa kuwa karibu kukamilisha mazungumzo ya kumsajili kiungo huyo mwenye umri wa miaka 17 na amewashukuru Lille kwa jukwaa walilompa.

"Wakati umefika wa mimi kukuaga. Asante sana kwa msaada wako usioyumba!" Sahabo aliandika katika mitandao yake ya kijamii.

Hakim Sahabo , Mchezaji wa timu ya taifa ya Rwanda
Hakim Sahabo , Mchezaji wa timu ya taifa ya Rwanda © Hakim Sahabo facebook

Sahabo alijiunga na Lille mnamo 2021 kutoka akademia ya KV Mechelen na kucheza katika timu ya U17 kabla ya kupandishwa kwenye timu ya U19 mnamo 2022.

Alifunga mabao matano katika msimu uliomalizika hivi punde huku Lille ikimaliza ya tano kwenye jedwali la Ligi ya Championnat ya U19.

Kinda huyo mwenye kasi ya ajabu anatarajiwa kuja Kigali Juni 16 kuisaidia timu ya taifa kuelekea mechi ya kufuzu AFCON dhidi ya Msumbiji Juni 18 kwenye Uwanja wa Huye.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.