Pata taarifa kuu

Philippe Diallo amechaguliwa kuwa rais mpya wa Shirikisho la Soka la Ufaransa

NAIROBI – Diallo ambaye amekuwa akishikilia majukumu ya uongozi wa muda katika shirikisho hilo baada ya kujiuzulu kwa kiongozi  wa muda mrefu Noel Le Graet, amechukua nafasi hiyo baada ya kushinda kwa zaidi ya asilimia 90 ya kura za wanachama  200 katika mkutano mkuu wa FFF mjini Paris.

Philippe Diallo amechaguliwa  kuwa rais mpya wa Shirikisho la Soka la Ufaransa
Philippe Diallo amechaguliwa kuwa rais mpya wa Shirikisho la Soka la Ufaransa AP - Michel Euler
Matangazo ya kibiashara

Philippe  mwenye umri wa miaka 59 anatarajiwa kuongoza shirikisho hilo hadi miwshoni mwa mwaka wa 2024.

Akizungumza baada ya uteuzi wake Diallo ameeleza kuwa hatua ya kuchaguliwa kwake ni heshima kubwa na kuwashukuru waliompigia kura.

Aidha amesema kuwa ni jukumu kubwa ambalo amepewa baadaya kile amesema kwamba wamevumilia katika nyakati ngumu katika miezi michache iliyopita.

Diallo alichukua nafasi ya kaimu rais mwezi Januari wakati Le Graet alipojiondoa kwa mara ya kwanza na kisha kulazimika kujiuzulu kufuatia shutuma za unyanyasaji wa kijinsia na kumaliza zaidi ya muongo mmoja wa uongozi wake katika shirikisho.

Noël Le Graët, aliyekuwa rais wa shirikisho la soka nchini Ufaransa
Noël Le Graët, aliyekuwa rais wa shirikisho la soka nchini Ufaransa AP - Christophe Ena

Hatua ya kujiuzulu kwa Le Graet kulikuja siku chache baada ya kuchapishwa kwa ripoti mbaya ya usimamizi katika shirikisho la FFF yenye makao yake makuu mjini Paris, ambayo ilikuwa imeagizwa na wizara ya michezo.

Wakati huo huo mchezo wa wanawake nchini Ufaransa ulikuwa unakabiliwa  na changamoto baada ya Corinne Diacre kutimuliwa kama kocha wa timu ya taifa wakati nafasi yake ilipodhoofika kufuatia uasi wa wachezaji wakuu.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.