Pata taarifa kuu

Faith Kipyegon wa Kenya ameandikisha rekodi mpya katika mbio za mita 1500

NAIROBI – Raia wa Kenya Faith Kipyegon aliweka rekodi mpya ya dunia ya mita 1500 katika mbio za Diamond League mjini Florence Italia  siku ya Ijumaa, huku Muingereza Laura Muir akimaliza katika nafasi ya pili.

Kipyegon baada ya kuweka rekodi mpya ya dunia na kushinda fainali ya wanawake ya mita 1500 REUTERS/Remo Casilli
Kipyegon baada ya kuweka rekodi mpya ya dunia na kushinda fainali ya wanawake ya mita 1500 REUTERS/Remo Casilli REUTERS - REMO CASILLI
Matangazo ya kibiashara

Kipyegon aliweka rekodi mpya baada ya kukimbia kwa dakika 3 sekunde 49.11, na kuvunja rekodi ya awali ya dakika 3:50 kwa mara ya kwanza, huku Muir akikimbia kwa muda bora wa msimu wa 3:57.09.

Ligi ya Diamond - Mwanariadha wa Kenya Faith Kipyegon akiwa na wanariadha wenzake wa kike baada ya kuwela rekodi mpya ya mbio za mita 1500  REUTERS/Remo Casilli
Ligi ya Diamond - Mwanariadha wa Kenya Faith Kipyegon akiwa na wanariadha wenzake wa kike baada ya kuwela rekodi mpya ya mbio za mita 1500 REUTERS/Remo Casilli REUTERS - REMO CASILLI

Genzebe Dibaba wa Ethiopia aliweka rekodi ya awali ya saa 3:50.07 mwaka 2015.

Ciara Mageean wa Ireland pia alikimbia wakati bora zaidi wa msimu alipomaliza wa nne kwa 4:00.95.

Viongozi mbalimbali kutoka nchini Kenya akiwemo rais William Ruto na kinara wa upinzani Raila Odinga wamempongeza mwanariadha huyo baada ya kuweka rekodi mpya ya mbio hizo.

Kipyegon ameshinda dhahabu ya dunia na Olimpiki mara mbili lakini hii ni mara yake ya kwanza kuvunja rekodi ya dunia.

Kipyegon bingwa wa mbio za mita 1500 duniani  REUTERS/Ciro De Luca
Kipyegon bingwa wa mbio za mita 1500 duniani REUTERS/Ciro De Luca REUTERS - CIRO DE LUCA

Sasa anashikilia mara ya kwanza na ya tatu kwa kasi zaidi katika historia, akitumia ubora wake wa awali wa 3:50.37 Agosti iliyopita.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.