Pata taarifa kuu

Barcelona ndio mabingwa wa La Liga

NAIROBI – Barcelona  inasherekea ushindi wao wa kwanza wa Ligue ya Uhispania tangu kuondoka kwa Lionel Messi katika klabu hiyo miaka miwili iliyopita wakati timu hiyo iliôkuwa inakabiliwa na changamoto za kifedha.

Barcelona ndio mabingwa wa La Liga msimu wa 2022-2023
Barcelona ndio mabingwa wa La Liga msimu wa 2022-2023 © Barcelona
Matangazo ya kibiashara

Kalbu hiyo ya Uhispania ilipata ushindi wa magoli manne kwa mawili dhidi ya Espanyol siku ya Jumapili katika mechi ambayo ilishuhudia mashabiki wa Espanyol kuingia katikati ya uwanja baada ya mechi, hali iliyowalazimu wachezaji wa Barcelona kuondoka.

Barcelona wameshinda ubingwa wa La Liga 2023
Barcelona wameshinda ubingwa wa La Liga 2023 © Barcelona

Robert Lewandowski alifunga mabao mawili, magoli yalioisadia klabu hiyo kupata taji lao la kwanza tangu mwaka wa 2019. Hatua hi ikija licha ya mechi nne kusalia kabla ya kumalizika kwa msimu.

Mara ya mwisho kwa Barcelona kusherehekea ushindi wa ligi bila ya kuwepo kwa Messi katika kikosi chake ilikuwa mwaka wa 1998-99.  Messi alijiunga na kikosi cha kwanza cha Barcelona mwaka wa 2004-05 na kisha kushinda taji la ligi msimu huo.

Barcelona players celebrate after the Spanish La Liga soccer match between Espanyol and Barcelona at the RCDE stadium in Barcelona, Sunday, May 14, 2023. (AP Photo/Joan Monfort)
Barcelona players celebrate after the Spanish La Liga soccer match between Espanyol and Barcelona at the RCDE stadium in Barcelona, Sunday, May 14, 2023. (AP Photo/Joan Monfort) AP - Joan Monfort

Sherehe za wachezaji wa klabu hiyo uwanjani baada ya mechi zilikatizwa baada ya tukio la mashabiki wa Espanyol kuingia uwanjani na kuaanza kuimba na kusherehekea na wachezaji hao.

Maofisa wa usalama walilazimika kuingilia tukio hilo kwa haraka kuwazuai mashabiki Zaidi kuingia.  Alejandro Balde na Jules Koundé pia nao waliifungia Barcelona, ambao kwa sasa wanamataji 27.

Ushindi huo dhidi ya mahisimu Espanyol uliwapa Barcelona alama 85 baada ya mechi 34, wakiwa pia na alama 14 zaidi ya Real Madrid, ambao waliwashinda Getafe kwa bao moja bila ya jibu siku ya Jumamosi.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.