Taji la klabu bingwa barani Afrika: CS Constantine yaongoza
CS Constantine ya Algeria ndio klabu pekee ambayo imepata ushindi katika mechi mbili ambazo imecheza hadi sasa, katika harakati za kuwania taji la klabu bingwa barani Afrika.
Imechapishwa:
Mwishoni mwa wiki iliyopita, CS Constantine iliishinda TP Mazembe ya DRC mabao 3-0 katika mechi yake ya pili iliyocheza nyumbani kayika uwanja wa Mohamed Hamlaoui.
Mechi ya kwanza, iliishinda Club Africain ya Algeria bao 1-0 mjini Sousse wiki mbili zilizopita.
Klabu hii inaongoza kundi la C kwa alama sita, ikifuatwa na Club Africain na TP Mazembe ambazo zina alama moja, huku Ismaily ya Misri ikiwa ya mwisho bila alama.
Matokeo mengine,
Kundi A:-
ASEC Mimosas (Ivory Coast) 1-0 Lobi Stars (Nigeria)
Mamelodi Sundowns (Afrika Kusini) 2-1 Wydad Casablanca (Morocco)
Kundi B:-
Esperiance de Tunis (Tunisia) 2-0 FC Platinum (Zimbabwe)
Orlando Pirates (Afrika Kusini) 3-0 Horoya (Guinea)
Kundi D:-
JS Saoura (Algeria) 1-1 Al-Ahly (Misri)
AS Vita Club (DRC) 5-0 Simba (Tanzania)