Pata taarifa kuu
RIPOTI-FIFA-Soka

Fifa yatoa ripoti ya mwezi ya viwango vya soka dunia

Timu ya taifa ya Colombia imechukua nafasi ya tatu kulingana na ripoti iliyotolewa alhamisi wiki hii na shirikisho la soka duniani Fifa, baad ya kuipiku timu ya taifa ya Uholanzi.

Mchezaji wa timu ya taifa ya Ujerumani,Toni Kroos (kushoto) na mchezaji wa timu ya taifa ya Argentina, Gonzalo Higuain katika fainali ya Kombe la dunia 2014.Julai 13 mjini Rio.
Mchezaji wa timu ya taifa ya Ujerumani,Toni Kroos (kushoto) na mchezaji wa timu ya taifa ya Argentina, Gonzalo Higuain katika fainali ya Kombe la dunia 2014.Julai 13 mjini Rio. Reuters / Eddie Keogh & Ueslei Marcelino - Montage / RFI
Matangazo ya kibiashara

Katika ripoti hiyo ya Fifa, Ujerumani inaongoza ikifuatiwa na Argentina, huku Uholanzi ikichukua nafasi ya nne baada ya kufungwa na timu ya taifa ya Czech mabao (2-1).

Timu ya taifa ya Ubelgiji imechukua nafasi ya tano ikiwa mbele ya Brazili na Uruguay, ambyo imechukua nafasi ya 7.

Kiungo wa Brazil, Neymar, wakati timu yake ilipoondolewa katika michuano ya Kombe la dunia 2014 ikiwa nyumbani.
Kiungo wa Brazil, Neymar, wakati timu yake ilipoondolewa katika michuano ya Kombe la dunia 2014 ikiwa nyumbani. REUTERS/Dominic Ebenbichler

Katika timu 10 bora, Brazil inachukua nafasi ya 6, Uhispania ikichukua nafasi ya 8, huku Ufaransa ikichukua nafasi ya 9 ikiwa mbele ya Uswisi.

Algeria ambayo ni moja ya mataifa ya Afrika yaliyoshiriki Kombe la dunia 2014, imechukua nafasi ya 20, ambapo Novemba mwaka 2012 ilichukua nafasi ya 19.

1. Ujerumani
2. Argentina
3. Colombia (+1)
4. Uholanzi (-1)
5. Ubelgiji

Mchezaji wa timu ya taifa ya Algeria, Sofiane Feghouli akifumbatiana na Islam Slimani, baada ya timu yao ya taifa kutinga katika mzunguuko wa nane, katika michuano ya Kombe la dunia 2014.
Mchezaji wa timu ya taifa ya Algeria, Sofiane Feghouli akifumbatiana na Islam Slimani, baada ya timu yao ya taifa kutinga katika mzunguuko wa nane, katika michuano ya Kombe la dunia 2014. REUTERS/Louafi Larbi

6. Brazil(+1)
7. Uruguay (-1)
8. Uhespania(-1)
9. Ufaransa(+1)
10. Uswiwi (-1)
11. Ureno
12. Chile
13. Italia (+1)
14. Ugiriki (-1)
15. Costa Rica
16. Mexico(+1)
17. Marekani (+1)
18. Uingereza(+2)
19. Croatia(-3)
20. Algeria (+4)
...

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.