Michuano ya Tennis ya French Open katika siku ya tatu
Leo ni siku ya tatu ya michuano ya Tennis ya French Open inayoendelea jijini Paris na Mwingereza Andy Murray ambaye ameshinda mataji mawili makubwa likiwemo lile la Wimbledon msimu uliopita, atashuka dimbani kumenyana na Andrey Golubev, kutoka Kazakhstan kwa upande wa wanaume katika mchezo wake wa kwanza.
Imechapishwa:
Upande wa wanawake bingwa wa Australian Open Li Na ameanza kutafuta ubingwa katika michuano hii dhidi ya Kristina Mladenovic wa Ufaransa.
Baadhi ya matokeo ya michuano ya jana Stanislas Wawrinka raia wa Usiwisi
alibanduliwa nje ya michuano hiyo katika mzunguko wa kwanza baada ya kufungwa na Mhispania Guillermo Garcia-Lopez kwa seti za 6-4, 5-7, 6-2, 6-0.
Rafael Nadal naye alimshinda Robby Ginepri wa Marekani kwa seti 6-0, 6-3, 6-0.
Mserbia Novak Djokovic akamfunga João Sousa wa Ureno kwa seti 6-1, 6-2, 6-4.
Kwa upande wa wanawake, Maria Sharapova kutoka Urusi amemshinda Mrusi mwezake Ksenia Pervak kwa seti 6-1, 6-2.