AFRIKA KUSINI-MAREKANI
Nyota wa Tennis nchini Marekani kutoa ujuzi kwa wanafunzi wa mchezo huo nchini Afrika Kusini
Watoto wadogo wanojifunza mchezo wa Tennis wanajiaandaa kupata mafunzo kutoka kwa vinara wa muda mrefu wa mchezo huo kutoka Marekani Serena Williams na mdogo wake Venus Williams katika mpambano utakaochezwa hii leo huko Soweto.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Timu mbili zenye wachezaji watano kwa kila timu zinatarajia kuvuta hisia za ulimwengu wakati wa mpambano baina ya ndugu hao wawili ambao wamekuwa wakifanya vizuri katika mchezo huo.
Nyota hao wa tennis nchini Marekani wako nchini Afrika Kusini kwa ziara ya kuhamasishamchezo huo miongoni mwa waafrika na hasa wasichana baada ya kufanya ziara ya aina hiyo nchini Nigeria mapema wiki hii.