Pata taarifa kuu

Washington yalaani 'mashambulizi ya kutowajibika' ya Iran Kurdistan ya Iraq

Marekani imelaani mashambulizi yaliyofanywa na Iran katika eneo la Kurdistan ya Iraq na kubaini kwamba "inapingana" na "mashambulio haya ya kiholela ya makombora" ambayo "yanahatarisha utulivu wa Iraq", kulingana na taarifa kutoka Idara ya Ulinzi.

Une vue générale d'Erbil, capitale de la région autonome du Kurdistan irakien. (Image d'illustration)
Muonekano wa Erbil, mji mkuu wa jimbo linalojitawala la Kurdistan ya Iraq. (Picha ya kielelezo) AFP - SAFIN HAMID
Matangazo ya kibiashara

Walinzi wa Mapinduzi ya Iran walitangaza mapema Jumanne kwamba wamerusha makombora kadhaa ya balestiki katika maeneo ya "kigaidi" huko Erbil, mji mkuu wa Kurdistan ya Iraq. Mashambulizi haya yaliua angalau "raia wanne" katika eneo hili linalojitawala la kaskazini mwa Iraq, kulingana na mamlaka za ndani.

Walinzi wa Mapinduzi ya Iran wamedai kulenga na kuharibu "makao makuu ya kijasusi" ambayo wamedai kuwa yalifanywa na Israeli, kama vile "muungano wa makundi ya kigaidi dhidi ya Iran" yalivyolengwa, kulingana na shirika la habari la IRNA.

Mamlaka za Kikurdi zinaripoti vifo vya takriban raia wanne. Miongoni mwa wahanga ni mfanyabiashara mashuhuri wa Kikurdi na familia yake nzima. Shughuli katika Uwanja wa ndege wa Erbil zimesitishwa. Katika taarifa kwa vyombo vya habari, Baraza la Usalama la Kurdistan linaishutumu Tehran kwa kutumia "madai yasiyo na msingi" kwa mashambulizi yake ya mara kwa mara dhidi ya eneo hilo. "Kilichotokea ni ukiukaji wa wazi wa uhuru wa eneo la Kurdistan na wa Iraq. Serikali ya shirikisho na jumuiya ya kimataifa haipaswi kukaa kimya mbele ya uhalifu huu,” imesema taarifa hiyo.

Kulingana na shirika la habari la IRNA, shambulio la Erbil linakuja kwa kulipiza kisasi mauaji ya hivi karibuni ya makamanda kadhaa wa Walinzi wa Mapinduzi, lakini pia ya viongozi wa "mhimili wa upinzani", jina lililopewa washirika wa Tehran katika vita vyake dhidi ya Israeli. Mnamo Januari 2, katika vitongoji vya kusini mwa Beirut, shambulio linalohusishwa na Israeli liliua naibu kiongozi wa kundi la Hamas, Saleh al-Arouri, na maafisa wengine sita na watendaji wa kundi hili la wanamgamo wa Kiislamu kutoka Palestina. Katikati ya mwezi wa Januari, Wissam Tawil, afisa mkuu wa kijeshi wa Hezbollah ya Lebanon, aliuawa kusini mwa Lebanon na shambulio pia lililohusishwa na Israeli.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.