Pata taarifa kuu

UN: Kambi zinazokinzana Yemen zaahidi kuheshimu usitishaji mpya wa mapigano

Mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa ametangaza siku ya Jumamosi, Desemba 23, kwamba waasi wa Houthi na serikali ya Yemen wamekubaliana kusitisha mapigano na wanafungua mchakato wa amani ili kumaliza mzozo huo.

Kutoka kushoto, Abdul-Qader el-Murtaza, mkuu wa ujumbe wa Houthi mjini Geneva, Hans Grundberg, mjumbe maalum wa Katibu Mkuu kwa Yemen, na Yahya Mohammed Kazman, anayewakilisha serikali ya Yemen, wakipeana mikono wakati wa fursa ya picha baada ya hitimisho la mkutano wa 7 wa Kamati ya Ufuatiliaji wa utekelezaji wa makubaliano ya kubadilishana wafungwa kwa Yemen, katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa ya Ulaya, huko Geneva, Jumatatu Machi 20, 2023.
Kutoka kushoto, Abdul-Qader el-Murtaza, mkuu wa ujumbe wa Houthi mjini Geneva, Hans Grundberg, mjumbe maalum wa Katibu Mkuu kwa Yemen, na Yahya Mohammed Kazman, anayewakilisha serikali ya Yemen, wakipeana mikono wakati wa fursa ya picha baada ya hitimisho la mkutano wa 7 wa Kamati ya Ufuatiliaji wa utekelezaji wa makubaliano ya kubadilishana wafungwa kwa Yemen, katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa ya Ulaya, huko Geneva, Jumatatu Machi 20, 2023. AP - Salvatore Di Nolfi
Matangazo ya kibiashara

Waasi wa Houthi na serikali ya Yemen wakiwa vitani, wameahidi tena kuheshimu makubaliano ya usitishaji vita na kukubali kufunguliwa kwa mchakato wa amani ili kumaliza mzozo huo, amesema mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa kwa Yemen amesema siku ya Jumamosi, Desemba 23.

Kufuatia mfululizo wa mikutano nchini Saudi Arabia na Oman, Hans Grundberg, "amekaribisha kujitolea kwa wahusika katika seti ya hatua zinazolenga kutekeleza kiwango cha nchi cha usitishaji vita […] na kushiriki katika maandalizi ya kuanzishwa tena kwa siasa jumuishi mchakato chini ya mwamvuli wa Umoja wa Mataifa,” ameeleza katika taarifa ya Umoja wa Mataifa.

Yemen ambayo ni nchi maskini zaidi kwenye rasi ya Arabia, imetumbukia kwa miaka minane katika vita kati ya waasi wa Houthi na vikosi vya serikali vinavyoungwa mkono tangu mwaka 2015 na muungano unaoongozwa na Saudi Arabia na hasa Falme za Kiarabu. Hata hivyo vurugu nchini humo zimepungua kwa kiasi kikubwa tangu makubaliano ya amani yaliyojadiliwa na Umoja wa Mataifa mwezi Aprili 2022, ambayo muda wake uliisha Oktoba mwaka jana lakini bado unaheshimiwa.

Kwa mujibu wa taarifa ya Umoja wa Mataifa, makubaliano hayo yanajumuisha ahadi za kulipa mishahara ya watumishi wa umma, kufungua barabara katika mji uliozuiliwa na waasi wa Taiz na maeneo mengine ya Yemen, na kuanza tena mauzo ya mafuta. "Wayemeni wanatarajia matokeo yanayoonekana kutoka kwa makubaliano haya mapya ili kupiga hatua kuelekea amani ya kudumu," amebainishaHans Grundberg. Ahadi ambazo "ni wajibu juu ya raia wa Yemeni", ameongeza.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.