Marekani: Iran ilihusika katika mashambulizi ya Houthi katika Bahari Nyekundu
Wahouthi wamelenga meli ambazo wanasema "zina uhusiano na Israeli" na kutishia kuvuruga biashara ya kimataifa. Iran imeripotiwa kutoa msaada katika kulenga meli hizo.
Imechapishwa:
Iran ilihusika katika mashambulizi ya Houthi katika Bahari Nyekundu, Marekani inasema.
"Hatuna sababu ya kuamini kwamba Iran inajaribu kuwazuia Houthi kuendelea na vitendo vyao vya kutowajibika," Marekani imeongeza. "Uungaji mkono wa Irani kwa Houthi ni thabiti na inatafsiriwa katika uwasilishaji wa zana za kisasa za kijeshi, usaidizi wa kijasusi, msaada wa kifedha na mafunzo," Marekani imesema, ikithibitisha kwamba Tehran "imewezesha" mashambulio haya wakati "ikiwakabidhi maamuzi ya operesheni kwa Houthi".
Bila msaada kutoka kwa Iran, waasi wa Yemeni "wangekuwa na ugumu wa kuona na kupiga" meli zinazozunguka katika Bahari ya Shamu, amesema mmoja wa serikali ya Marekani.
Iran, mfuasi wa Houthi
Wimbi hili la mashambulizi, linalofanywa na ndege zisizo na rubani na makombora dhidi ya meli ambazo Wahouthi wanaamini kuwa "zina uhusiano na Israeli", linatishia kuvuruga biashara ya kimataifa. Kampuni kuu za usafiri wa baharini kwa kweli zimeacha kutumia Mlangowa Bahari wa Bab el-Mandeb.
Waasi wa Houthi ambao wanadhibiti sehemu kubwa ya Yemen lakini hawatambuliwi na jumuiya ya kimataifa, wanarudia kusema kwamba wataendelea maadamu chakula na dawa hazitarudi kwa wingi wa kutosha katika Ukanda wa Gaza, eneo la Palestina lililoshambuliwa kwa mabomu na kuzingirwa na Israel. kujibu shambulio ambalo halijawahi kufanywa na Hamas mnamo Oktoba 7 kwenye ardhi ya Israeli.
Iran inatambua uungaji mkono wake wa kisiasa kwa Wahouthi, katika vita tangu mwaka 2014 dhidi ya serikali ya Yemeni inayotambuliwa na jumuiya ya kimataifa. Lakini Tehran inakanusha kutoa vifaa vya kijeshi kwa waasi.
Muungano wa nchi kumi
Ili kukabiliana na mashambulizi "ya kutowajibika" ya waasi wa Houthi katika bahari ya Shamu, Lloyd Austin, Waziri wa Ulinzi wa Marekani, alitangaza Jumatatu kuundwa kwa muungano wa kimataifa unaoundwa na nchi kumi, ambazo ni Ufaransa, Uingereza, Bahrain, Kanada, Italia, Uholanzi, Norway, Uhispania na Visiwa vya Shelisheli.
Bahari ya Shamu ni "barabara kuu ya bahari" inayounganisha Bahari ya Mediterania na Bahari ya Hindi, na kwa hiyo Ulaya hadi Asia. Karibu meli 20,000 hupitia Mfereji wa Suez kila mwaka, mahali pa kuingilia na kutoka kwa meli zinazopitia Bahari Nyekundu.
Ikiwa hazitapitia tena Mfereji wa Suez na Bahari Nyekundu, meli zitalazimika kuzunguka Afrika na kupitia Rasi ya Tumaini Jema, ambayo itarefusha safari.