Pata taarifa kuu

Syria: UN yaona masharti ya Damascus kupitisha misaada mpakani 'hayakubaliki'

Umoja wa Mataifa una wasiwasi kuhusu 'masharti yasiyokubalika' yaliyotolewa na Damascus kutumia kivuko cha mpaka cha Bab al-Hawa kupeleka misaada ya kibinadamu katika maeneo ya waasi kaskazini magharibi mwa Syria, kulingana na waraka ambao uliosomwa na shirika la habari la AFP siku ya Ijumaa.

Kambi ya Karama ya wakimbizi wa ndani wa Syria waliokimbia makazi yao mnamo Februari 14, 2022, karibu na kijiji cha Atmeh katika mkoa wa Idlib nchini Syria.
Kambi ya Karama ya wakimbizi wa ndani wa Syria waliokimbia makazi yao mnamo Februari 14, 2022, karibu na kijiji cha Atmeh katika mkoa wa Idlib nchini Syria. © Omar Albam / AP Photo
Matangazo ya kibiashara

Barua kutoka kwa mamlaka ya Syria inayoruhusu utumiaji wa sehemu hii ya mpakani kati ya Uturuki na Syria "ina masharti mawili yasiyokubalika", imebaini hati iliyowasilishwa kwa Baraza la Usalama siku ya Ijumaa na Ofisi ya Uratibu wa Masuala ya Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa (OCHA) , ambayo inasema ina wasiwasi kuhusu marufuku yaliyowekwa kuzungumza na mashirika "yaliyotajwa kama 'magaidi'" na "usimamizi" wa shughuli zake na mashirika mengine.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.