Pata taarifa kuu

Afghanistan: Kampuni ya China yatia saini mkataba wa uchimbaji mafuta na Taliban

Mkataba wa kwanza wa kimataifa wa uchimbaji mafuta ulitiwa saini mjini Kabul siku ya Alhamisi tarehe 5 Januari. Hundi ya dola milioni 750 ambayo itaiwezesha Beijing kutafuta mafuta kaskazini mwa Afghanistan na ambayo inaupa utawala mpya wa Afghanistan uwekezaji wa kigeni na maonyesho ya kimataifa unaohitaji.

Msemaji wa Taliban Zabihullah Mujahid mjini Kabul tarehe 17 Agosti 2021.
Msemaji wa Taliban Zabihullah Mujahid mjini Kabul tarehe 17 Agosti 2021. REUTERS - STRINGER
Matangazo ya kibiashara

Makubaliano hayo yanataka kampuni ya Xinjiang Asia ya Kati ya Petroli na Gesi (CAPEIC) kuchimba mafuta katika bonde la Amu Darya, kulingana na BBC.

Taliban wameshinda yote

Kwenye karatasi, Taliban wameshinda kila kitu. Tangu kudhibitiwa kwa mji mkuu wa Afghanistan, Kabul, wamekuwa wakitafuta pesa. Mkataba huo unatoa mrahaba wa 15% unaolipwa kwa utawala wa Afghanistan kwa kipindi cha miaka ishirini na mitano. Walitaka miundombinu mipya. China imekubali kujenga kiwanda cha kwanza cha kusafisha mafuta nchini Afghanistan. Jambo ambalo pia litatoa ajira. Kulingana na mamlaka ya Taliban, watu 3,000 kutoka eneo hilo watahusishwa na mradi huu.

Utakuwa mkataba wa kwanza mkubwa wa uchimbaji wa nishati na kampuni ya kigeni tangu Taliban kuchukua udhibiti wa Afghanistan mnamo 2021.

Kujitosheleza

Kampuni ya kitaifa ya mafuta ya China, ambayo ilianza shughuli zake nchini Afghanistan mwaka 2012, haitaki kuacha sehemu yake ya soko. Na haijalishi nani anatawala. Uzuri wa mkataba huu, kwa mujibu wa balozi wa China aliyekuwepo wakati wa kutiwa saini, ni kuweka uchumi wa Afghanistan kwenye njia ya kujitosheleza.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.