Pata taarifa kuu
AFGHANISTAN

Marekani yatishia kuendelea kuilenga Taliban ikiwa itaendelea na mashambulizi

Marekani inasema jeshi lake litaendelea kutekeleza mashambulizi ya angaa nchini Afghanistan kufuatia ongezeko la mashambulizi ya kundi la Taliban, wakati huu  vikosi vya mwisho vikijiandaa  kuondoka nchini humo ifikapo tarehe 11 mwezi Septemba mwaka huu.

Jenerali Kenneth McKenzie, ambaye anaongoza taasisi ya ulinzi wa vikosi vya Marekani, Afghanistan, katika mkutano na waandishi wa habari huko Kabul Julai 25, 2021.
Jenerali Kenneth McKenzie, ambaye anaongoza taasisi ya ulinzi wa vikosi vya Marekani, Afghanistan, katika mkutano na waandishi wa habari huko Kabul Julai 25, 2021. REUTERS - STAFF
Matangazo ya kibiashara

Hata hivyo, jeshi la Marekani halijasema iwapo litaendelea kutekeleza mashambulizi hayo ya angaa baada ya kuondoka nchini humo.

Rais Biden alisema kuwa tarehe 31 mwezi Agosti ndio itakuwa “siku yetu ya mwisho hapa, baada ya siku hiyo tutaendelea kutoa misaada muhimu kwa jeshi la Afghanistan hasa, jeshi la angaa, kwa hivyo msaada huo utaendelea hata baada ya tarehe 31 mwezi Agosti.

Kumeshuhudiwa ongezeko la uasi kutokana na mashambulizi ya wanamgambo wa Taliban ambao pia wamedhibiti mipaka muhimu, wilaya kadhaa na kuizingira baadhi ya miji mikuu ya majimbo tangu mapema mwezi Mei, wakati muungano wa wanajeshi wa kigeni unaoongozwa na Marekani ulipoanza kuondoka nchini humo.

Taarifa ya wizara ya mambo ya ndani ya Afghanistan imesema "ili kukabiliana na machafuko na kuzuia vuguvugu la wanamgambo wa Taliban, kumeanzishwa zuio la watu kutotembea nje kwenye majimbo 31 nchini humo," kasoro Kabul, Panjshir na Nangarhar.Watu hawataruhusiwa kutembea kuanzia saa nne usiku hadi saa kumi za alfajiri kwa saa za nchini Afghanistan, amesema msemaji wa wizara hiyo ya mambo ya ndani Ahmad Zia Zia, kwenye taarifa ya sauti iliyosambazwa kwa waandishi wa habari.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.