AFGHANISTANI
Taliban kuanza tena mashambulizi dhidi ya Wamarekani
Kundi la Taliban limetishia kuanza tena mashambulizi dhidi ya wanajeshi wa Marekani nchini Afghanistan ikiwa hawataondoka nchini humo kwa tarehe iliyopangwa Mei 1.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Siku ya Alhamisi, rais wa Marekani Joe Biden alisema itakuwa vigumu kwa jeshi la Marekani kuheshimu tarehe ya mwisho iliyokubaliwa mwaka jana kati ya waasi na Washington.
Katika taarifa, Taliban wamesema "watalazimika kuendelea na jihadi yao na mapambano yao ya silaha dhidi ya vikosi vya kigeni kuikomboa nchi yao" ikiwa tarehe ya Mei 1 haitazingatiwa.