Marekani kuichukulia vikwazo Iran kutokana na ukandamizaji dhidi ya waandamanaji
Marekani inatarajia kuchukuwa vikwazo wiki ijayo dhidi ya maafisa wa Irani kwa kuhusika kwao katika ukandamizaji mkali wa maandamano ya mwaka jana dhidi ya serikali nchini Iran, vyanzo vitatu rasmi vimebaini.
Imechapishwa:
Kulingana na moja ya vyanzo hivyo, vikwazo hivyo, vinalenga watu kadhaa na kambuni kadhaa za Irani.
"Ikiwa hii itathibitishwa, itaonyesha tu kutapa tapa kwa utawala ambao uadui wao kwa watu wa Irani unajulikana," Alireza Miryousefi, msemaji wa ujumbe wa Irani kwa Umoja wa Mataifa huko New York amesema katika taarifa.
Karibu watu 1,500 waliuawa katika kipindi kisichozidi wiki mbili baada ya maandamano kuanza mnamo Novemba 15, 2019, kulingana na shirika la habari la REUTERS, ikinukuu maafisa watatu kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani ya Iran.