Pata taarifa kuu
ISRAEL-PALESTINA-MAUAJI

Askari wa Israel wamuua raia mmoja wa Palestina

Wanajeshi wa Israel wamempiga risasi na umuua mwanaume wa Kipaletina, aliyekataa kukamatwa katika eneo la ukingo wa Magharibi.

Askari wa Israel wakimkagua Mpalestina katika mji wa al-Fawar, Ukingo wa Magharibi Agosti 16, 2016.
Askari wa Israel wakimkagua Mpalestina katika mji wa al-Fawar, Ukingo wa Magharibi Agosti 16, 2016. AFP
Matangazo ya kibiashara

Wizara ya afya ya Palestina imemtambua mwanaume aliyeuawa kuwa Mohammed Saraheen, mwenye urmi wa miaka 30.

Israel haijaeleza ni kwanini ilikuwa inataka kumkamata raia huyo wa Palestina lakini hapo awali imekuwa ikisema kuwa raia wake wameendelea kulengwa na Wapalestina na hata kuwajeruhi na kuwauawa.

Mwezi Oktoba mwaka uliopita zaidi ya watu 200 walipoteza maisha katika makabiliano kati ya Israel na Palestina katika ukingo huo wa Magharibi.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.