ISRAEL-PALESTINA-MAUAJI
Askari wa Israel wamuua raia mmoja wa Palestina
Wanajeshi wa Israel wamempiga risasi na umuua mwanaume wa Kipaletina, aliyekataa kukamatwa katika eneo la ukingo wa Magharibi.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Wizara ya afya ya Palestina imemtambua mwanaume aliyeuawa kuwa Mohammed Saraheen, mwenye urmi wa miaka 30.
Israel haijaeleza ni kwanini ilikuwa inataka kumkamata raia huyo wa Palestina lakini hapo awali imekuwa ikisema kuwa raia wake wameendelea kulengwa na Wapalestina na hata kuwajeruhi na kuwauawa.
Mwezi Oktoba mwaka uliopita zaidi ya watu 200 walipoteza maisha katika makabiliano kati ya Israel na Palestina katika ukingo huo wa Magharibi.