Pata taarifa kuu
ISRAELI-PALESTINA-Usalama

Taharuki yatanda kwenye eneo la Jerusalem

Saa chache baada ya kutekwa na kisha kuuawa kwa mtoto mmoja raia wa Palestina, hali imezidi kuwa tete kwenye eneo la Jerusalem kufuatia makabiliano kati ya wanajeshi wa Israel na vijana wa Kipalestina.

Makabilianao kati ya raia wa Palestina na wanajeshi wa Israeli, baada ya kukotwa kwa muili wa kijana wa kipalestina aliechomwa moto karibu na msitu moja nchini Israeli.
Makabilianao kati ya raia wa Palestina na wanajeshi wa Israeli, baada ya kukotwa kwa muili wa kijana wa kipalestina aliechomwa moto karibu na msitu moja nchini Israeli. REUTERS/Ammar Awad
Matangazo ya kibiashara

Tukio la kutekwa na kisha kuuawa kwa kijana wa Kipalestina linajiri wakati huu ambapo polisi nchini Israel wanaendelea na uchunguzi kuhusu tukio la kuuawa kwa vijana watatu raia wa Israel ambao walitekwa na kuuawa na kisha miili yao kitelekezwa kwenye msitu wa Jerusalem.

Makabiliano yakiendelea kati ya raia wa Palestina na vikosi vya Israeli.
Makabiliano yakiendelea kati ya raia wa Palestina na vikosi vya Israeli. REUTERS/Mohamad Torokman

Hii leo kwa siku ya pili mfululizo, ndege za Israel zimeendelea na mashambulizi yake kwenye eneo la ukanda wa gaza hasa kwenye ngome za kundi la Hamas, ambalo Israel inadai ndilo limehusika na mauaji ya raia wake watatu.

Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu ametoa wito kwa pande zote mbili kutojiingiza kwenye mapigano wala vurugu wakati huu ambapo kumekuwa na hali ya sintofahamu kati ya raia wa Israel na Palestina.

Waziri mkuu wa Israeli Benjamin Netanyahu.
Waziri mkuu wa Israeli Benjamin Netanyahu. Reuters/Jim Hollander/Pool

Jumuiya ya kimataifa imelaani tukio la kuuawa kwa kijana wa Kipalestina na kuonya kuhusu kuendelea kushuhudiwa kwa matukio haya ya utekaji nyara ambayo inasema yanachochea kudhoofisha upatikanaji wa amani kati ya Israeli na Palestina.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.