Mji wa Ivory Coast wadaiwa kuwa ni eneo la Kisumu nchini Kenya
Imechapishwa:
Cheza - 10:00
Mwezi uliopita kuna picha iliibuka mtandaoni ikidai kuonesha mji huo ulio kando ya ziwa ukionekana nadhifu.
Lakini dai hili ni la uongo. Picha halisi ni ya mji wa Abidjan ambao ndio mkubwa na wa kibiashara wa Côte d'Ivoire katika chapisho hili la Januari 25 mwaka huu.
Picha hii inaonesha gari kwenye barabara kuu na mandhari yake ni mji, pia bendera zimewekwa kando ya barabara na mtumizi mmoja wa facebook mfano alisema “tunaita Ulaya, Kisumu ndio mji mzuri wa kutembelea nchini kenya, Afrika Mashariki na Afrika.
Kwa kifupi tu mji wa Kisumu msikilizaji ndio wa tatu kwa ukubwa baada ya Nairobi na Mombasa, na kupitia usafiri wa maji na reli, sasa mji huo umegeuka kuwa kitovu cha kibiashara, viwanda na usafiri.