Video ya zamani inayodai hosipitali jijini Nairobi imefurika kutokana na mvua kubwa
Imechapishwa:
Cheza - 10:16
Moja ya habari potofu tunaangazia wiki hii ni video ya hospitali moja nchini Kenya kufurika ikidaiwa ni y a mwaka huu lakini video ni ya mwaka 2019.
Mvua imekuwa ikinyesha sana nchini Kenya lakini pia haswa jiji kuu la Nairobi. Mvua ya Januari 5 mwaka huu ilisababisha mafuriko makubwa na hata baadhi ya barabara hazikuwa zinapitika
Watumizi wa mitandao ya kijamii walisambaza vídeo ya hospital hiyo kufurika, baadhi ya wengine wakidai ni hospitali ya Aga Khan huku wengine wakisema ni hospitali ya Nairobi.
Hata hivyo madai haya yanapotosha. Ndio hii video ni ya hospitali ya Aga Khan japo ilichukuliwa mwaka 2019.