Nchini Kenya baada ya bunge kupokea ombi mnamo Agosti 2023 lililopendekeza kupigwa marufuku kwa mtandao wa TikTok kwa madai kuwa mtandao huu unakuza maudhui yasiyofaa, machapisho yaliibuka mtandaoni yakidai kuwa nchi hiyo ilikuwa imepiga marufuku TikTok na vilevile Telegram.
Matangazo ya kibiashara
Lakini madai hayo ni ya uongo: Mamlaka ya Mawasiliano ya Kenya (CAK) iliiambia AFP Fact Check kwamba majukwaa hayo mawili bado yalikuwa yanafanya kazi nchini.
Nasi katika uchunguzi wetu tunaona hapa mtandao wa TiktTok na Telegram, zote zinafanya kazi. Ni dhahiri shairi kuwa hazijapigwa marufuku.