Pata taarifa kuu
TANZANIA-CORONA-AFYA-UCHUMI

Tanzania yalegeza baadi ya vizuizi vya safari za ndege

Serikali ya Tanzania imelegeza marufuku dhidi ya safari za ndege za kimataifa, kwa kile mamlaka zimesema ni kutokana na uongezeko la mahitaji ya huduma muhimu.

Mji mkuu wa uchumi wa Tanzania, Dar es Salaam ambo pia inakabiliwa na janga la Corona.
Mji mkuu wa uchumi wa Tanzania, Dar es Salaam ambo pia inakabiliwa na janga la Corona. Wikimedia/Chen Hualin
Matangazo ya kibiashara

Hamza Johari, mkurugezi wa huduma za Ndege nchini humo amesema hilo limeafikiwa kutokana maombi ya kutaka kulegeza masharti hayo,ili ndege za kutoa hudumu muhimu kama vile usafirishaji wa  dawa ziruhusiwi kupaa.

Wakati huo huo serikali ya Zambia imechukua hatua ya kufunga mpaka wake na nchi jirani ya Tanzania kuanzia leo Jumatatu kwa kukabiliana na maambukizi ya virusi vya Corona. Hii ni baada ya kuwa na maambukizi mengi, hususan miongoni mwa wafanyabiashara wa ngono na madereva wa Malori kwenye miji ya mipaka nchini humo.

Akizungumza kwa niaba ya rais wa taifa hilo, Edgar Lungu Waziri wa afya nchini humo Chitalu Chilufya ametangaza kwamba mpaka huo utafungwa kwa muda .

Amesema kwamba hatua hiyo itatoa fursa kwa mikakati mipya ya kukabiliana na virusi hivyo kuwekwa.

Katika muda huo, amesema wafanyakazi wa uhamiaji katika mpaka huo watapatiwa mafunzo mapya ya jinsi ya kuhudumia mizigo na raia wanaoingia.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.