Pata taarifa kuu
SUDANI-KUSINI-SIASA-USALAMA

Sudani Kusini: Kiir na Mashar wakubaliana kuunda serikali ya muungano

Viongozi wa Sudan Kusini, rais Salva Kiir na mpinzani wake Riek Machar, wamekubaliana kuunda serikali ya muungano Jumamosi Februari 22, 2020.

Kiongozi wa waasi Riek Machar (kushoto) na rais wa Sudani Kusini Salva Kiir wakisaini makubaliano ya kugawana madaraka huko Khartoum, Sudani, Agosti 5, 2018.
Kiongozi wa waasi Riek Machar (kushoto) na rais wa Sudani Kusini Salva Kiir wakisaini makubaliano ya kugawana madaraka huko Khartoum, Sudani, Agosti 5, 2018. REUTERS/Mohamed Nureldin Abdallah
Matangazo ya kibiashara

Wawili hao wamekubaliana hili baada ya mazungumza ya saa kadhaa katika ikulu ya Juba Alhamisi wiki hii.

Tangazo hilo ni hatua kubwa katika kupatikana kumalizika kwa vita vya wenyewe kwa wenywe nchini humo vilivyodumu kwa miaka mitano na kuwaua karibu watu 400,000 na kuliharibu kabisa taifa hilo changa kabisa duniani.

Marekani imepongeza hatua hii na kusema Washington iko tayari kuunga mkono serikali hiyo ambayo itamrejesha Machar kama makamu wa kwanza wa rais.

Matumaini ya kuundwa kwa serikali hii yalionekana baada ya rais Kiir kukubali shinikizo za kupunguza idadi ya majimbo kutoka 32 hadi 10.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.