Pata taarifa kuu
BURUNDI-SIASA-USALAMA

Upinzani ulio uhamishoni kushiriki mazungumzo ya amani ya Burundi Arusha

Wanasiasa wa Burundi waishio uhamishoni wamesema watakuwa tayari kushiriki katika mazungumzo ya kusaka suluhus ya mzozo wa Burundi yalioitishwa na mratibu wa mazungumzo hayo rais wa zamani wa Tanzania Benjamin William Mkapa kuanzia Oktoba 18 hadi Oktoba 24 mjini Arusha nchini Tanzania.

Kiongozi wa muungano wa vyama vya kisiasa vya upinzani Cnared, Jean Minani (wa pili kutoa kushoto).
Kiongozi wa muungano wa vyama vya kisiasa vya upinzani Cnared, Jean Minani (wa pili kutoa kushoto). CNARED Burundi/twitter.com
Matangazo ya kibiashara

Muungano wa wanasiasa waishio uhamishoni Cnared unasema utakuwa tayari kushiriki kwenye mazungumzo hayo ambayo hata hivyo yanakosolewa vikali na baadhi ya mashirika ya kiraia ambayo yanasema hayajaona utashi wowote kutoka kwa serikali ya rais Pierre Nkurunziza kutaka kumaliza mzozo wa kisiasa uliopo.

Onesime Nduwimana msemaji wa muungano wa vyama vya upinzani (Cnared) anaona itakuwa ni fursa nzuri kuona mazungumzo hayo yanawashirikisha wadau wote katika mgogoro wa Burundi, vinginevyo itakuwa ni kupoteza muda na kwamba Warundi wana matarajio makubwa kutoka kwa wadau wote wa kisiasa.

Mashirika kadhaa ya kiraia yanaona kuwa mzungumzo hayo yajayo hayatakuwa suluhu ya mzozo uliopo ukizingatia kuwa serikali ya Burundi bado hainaonyesha umuhimu wa kuzungumza na wapinzani wake.

Serikali ya Burundi imekuwa ikipinga kuketi kwenye meza ya mazungumzo na wanasiasa hao kutoka Cnared ikiwashtumu kwamba baadhi yao walihusika katika jaribio la mapinduzi lililotibuliwa Mei 15, 2015.

Machafuko nchini Burundi yamesababisha zaidi ya watu 2000 kuawa kwa mujibu wa mashirika ya haki za binadamu nchini Burundi na maefu kadhaa kutoroka makazi yao na kukimbilia katika nchi jirani.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.