Pata taarifa kuu
TANZANIA-UN-DRC-USALAMA

Miili ya askari wa Tanzania kurejeshwa nyumbani wiki hii

Jeshi la Tanzania limethibitisha kupoteza askari 15 waliouawa katika shambulio lililoendeshwa na watu wenye silaha wanasadikiwa kuwa waasi wa Uganda wa ADF katika kambi ndogo mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Askari wa kikosi maalum ktoka Tanzania wakiingia kwenye maficho ya waasi wa Kihutu wa Rwanda wa FDLR,wakati wa operesheni BRONCO, Desemba 2016, katika msitu wa KALIMA (RUTSHURU), mashariki mwa DRC.
Askari wa kikosi maalum ktoka Tanzania wakiingia kwenye maficho ya waasi wa Kihutu wa Rwanda wa FDLR,wakati wa operesheni BRONCO, Desemba 2016, katika msitu wa KALIMA (RUTSHURU), mashariki mwa DRC. MONUSCO Forces/FIB-TANZBATT
Matangazo ya kibiashara

Katika shambulio hilo askari zaidi ya arobaini walijeruhiwa na kwa sasa wanapewa matibabu.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Majeshi ya Tanzania jini Dar es Salaam, Mnadhimu Mkuu wa jeshi hilo, Luteni Jenerali James Mwakibolwa amesema majeruhi 44 bado wanaendelea vizuri na taratibu za kusafirisha miili hadi Dar es Salaam zinaendelea baina ya serikali ya Tanzania na Umoja wa Mataifa.

Amesema miili hiyo inatarajiwa kusafirishwa mapema wiki hii, Jumanne au Jumatano.

Luteni Jenerali Mwakibolwa alisem awalizipokea taarifa za fivo vya askari hao kwa masikitiko, lakini amesem ahawatavunjika moyo wala kutetereka.

Alisema jeshi la Tanzania litasimama imara kwa kutetea na kulinza amani kwa ushirikiano na Umoja wa Mataifa.

Askari wa Tanzania wanaojumuika katika kikosi cha Umoja aw Mataifa walivamiwa na waasi wa Uganda wa ADF Desemba 7 jioni katika eneo moja liliopo kaskazini mashariki mwa mji wa Beni, mashariki mwa DRC.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.