Pata taarifa kuu
KENYA-UCHAGUZI

Raila Odinga : Niko tayari kufichua wizi wa kura

Wakati ambapo hali ya utulivu ikianza kurejea nchini Kenya, kiongozi wa upinzani nchini Kenya Raila Odinga akihojiwa na gazeti la Financial Times la Uingereza amesema kwamba atafichua ushahidi siku ya Jumanne kuhusu vile alivyoibiwa kura.

Kiongozi wa upinzani nchini Kenya Raila Odinga.
Kiongozi wa upinzani nchini Kenya Raila Odinga. REUTERS/Thomas Mukoya
Matangazo ya kibiashara

Bwana Odinga amedai kwamba wadukuzi waliingilia kompyuta za tume ya Uchaguzi na kuweka hesabu ambazo zilimpatia ushindi rais Uhuru Kenyatta.

“Niko tayari kuonyesha jamii ya kimataifa na Wakenya jinsi gani tulivyoibiwa kura zetu, “ amesema Bwa Odinga .

Raila Odinga ambaye alikuwa akiwania urais kwa mara ya nne alishindwa katika uchaguzi huo wa urais uliyofanyika Agosti 8, 2017. Pia alibaini kwamba hatowania tena urais , huku akisema aliwataka Wakenya kujua kilichofanyika wakati wa uchaguzi huo.

“Natangazia Wakenya kwamba sitawania tena urais. Tumependelea tu Wakenya kujua mchezo uliopigwa katika uchaguzi wa urais wa mwaka 2017. Sio swala la kuwa mbifansi, Sio swala kuhusu Raila Odinga, “ ameongeza Raila Odinga.

Wakati huo huo Tume ya Uchaguzi imefutilia mbali madai hayo ikibaini kwamba ni madai yasiokuwa na msingi.

Machafuko ya hivi karibuni nchini Kenya yamesababisha vifo kadhaa na watu kadhaa kujeruhiwa na wengine kukamatwa.

Vikosi vya usalama katika eneo la Kibera mjini Nairobi, ambapo mvutano na makabiliano vilishuhudiwa siku ya Jumamosi, Agosti 12, 2017.
Vikosi vya usalama katika eneo la Kibera mjini Nairobi, ambapo mvutano na makabiliano vilishuhudiwa siku ya Jumamosi, Agosti 12, 2017. MARCO LONGARI / AFP

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.