Pata taarifa kuu
TANZANIA

Rais Magufuli aagiza kufutwa kazi kwa watumishi wa umma karibu 10,000

Rais wa Tanzania John Magufuli ameagiza kufutwa kazi kwa zaidi ya wafanyikazi wa karibu 10,000.

Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli, Dar es Salaam, Novemba 4, 2016.
Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli, Dar es Salaam, Novemba 4, 2016. Screenshot/Azama TV
Matangazo ya kibiashara

Magufuli ametoa tangazo hili siku ya Ijumaa baada ya kupokea ripoti kuhusu uchunguzi wa wafanyikazi wa serikali  waliotumia vyeti gushi ili  kupata kazi serikalini.

Aidha, ameitaka Wizara ya Fedha kutowalipa mshahara wafanyikazi hao waliobainika kuwa na vyeti hivyo baada ya uchunguzi kufanyika.

Kiongozi huyo ametaka majina ya wafanyikazi hao kuchapishwa katika magazeti ya nchini hiyo huku walioathirika wakitakiwa kuacha kazi mara moja.

“Watakaokataa kuondoka ikifika mwezi wa tano, watakumbana na mkono wa sheria na watafungwa jela miaka saba,” alisema Magufuli.

Katika hatua nyingine, Magufuli amesema kuwa hivi karibuni serikali yake  itatangaza nafasi mpya 52,000 za kazi kwa raia wa nchi hiyo ya Afrika Mashariki.

Uamuzi huu wa rais Magufuli unakuja wakati huu dunia ikitarajiwa kuadhisha sikukuu ya Wafanyikazi tarehe 1 mwezi Mei, wiki ijayo.

Tanzania ni mojawapo ya nchi za bara la  Afrika inayoendelea kukabiliwa na changamoto ya ajira haya kwa vijana.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.