Pata taarifa kuu
TANZANIA-HAKI-SHERIA

Serikali ya Tanzania yawataka wapenzi 3 wa jinsia moja kuripoti polisi

Wizara ya Afya nchini Tanzania imewataka watu watatu inaowashutumu kuwa wapenzi wa jinsia moja kuripoti polisi kwa mijali ya kuhojiwa na iwapo hawatofanya hivyo watakamwa.

Agosti 9, wanaharakati wanaotetea haki za mashoga bchini Uganda waliandamana kwa kukaribisha uamuzi wa kutosahihisha  sheria ya kupambana na mashoga.
Agosti 9, wanaharakati wanaotetea haki za mashoga bchini Uganda waliandamana kwa kukaribisha uamuzi wa kutosahihisha sheria ya kupambana na mashoga. REUTERS/Edward Echwalu
Matangazo ya kibiashara

Naibu waziri wa afya nchini humo Hamis Kingwangalae amebaini kwamba wizara yake inawashtumu watu hao kuambaza harakati za wapenzi wa jinsia moja kupitia mitandao ya kijamii kinyume na sheria.

Vitendo vya wapenzi wa jinsia moja ni kinyume na sheria nchini Tanzania na watu wanaokabiliwa na hatia hiyo, wanapaswa kupewa adhabu ya kifungo cha hadi miaka 30 jela.

Serikali imetishia kupiga marufuku makundi ambayo yanaunga mkono haki za watu wa mapenzi ya jinsia moja.

Itakumbukwa kwamba mwaka uliopita, Waziri wa Afya alitangaza kwamba mpango wa kuwapatia matibabu wapenzi wa jinsia moja walio na virusi vya HIV utasimamishwa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.