Pata taarifa kuu
UGANDA-SOMALIA

Uganda kuondoa wanajeshi wake nchini Somalia mwaka ujao

Jeshi la Uganda linasema litaanza kuwaondoa wanajeshi wake wanaopambana na kundi la Al Shabab nchini Somalia mwaka ujao.

Baadhi ya wanajeshi wa kikosi cha Uganda wanaounda jeshi la AMISOM nchini Somalia
Baadhi ya wanajeshi wa kikosi cha Uganda wanaounda jeshi la AMISOM nchini Somalia Reuters
Matangazo ya kibiashara

Uganda ilikuwa nchi ya kwanza barani Afrika kutuma kikosi chake nchini humo mwaka 2007, chini ya mwavuli wa AMISOM kwa lengo la kuilinda serikali iliyokuwa inaungwa mkono na Jumuiya ya Kimataifa.

Mkuu wa jeshi hilo la UPDF, Jenerali Katumba Wamala hajasema sababu kuu ya wanajeshi wa nchi yake kuondoka Somalia, ila amesema tu wakati hufika na mtu hurudi nyumbani.

Kuelekea kurejea kwa jeshi hilo la Uganda, limeendelea kushirikiana na Burundi, Djibouti, Ethiopia na Kenya kupambana na wanamgambo hao.

Mwezi uliopita, msemaji wa jeshi Paddy Ankunda alinukuliwa akisema jeshi la nchi hiyo lipo kwenye harakati za kurudi nyumbani.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.