UGANDA-USALAMA
Watu 29 watekwa nyara Uganda
Watu wasiofahamika wakiwa wamejihami kwa silaha wamewateka watu 29 katika Wilaya ya Yumbe nchini Uganda, karibu na mpaka wa Sudan Kusini.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Matangazo ya kibiashara
Ripoti zinasema kuwa utekaji nyara huo ulifanyika mapema wiki hii.
Mwenyekiti wa Wilaya hiyo Taban Yasiin anasema kuwa watu hao huenda wamepelekwa nchini Sudan Kusini.
Kabla ya utekeaji nyara huo, kundi hilo la watu lilivamia wilaya nyingine ya Moyo na kuiba mifugo na vyakula kutoka kwa familia mbalibali.