Pata taarifa kuu

Usalama waimarishwa nje ya ubalozi wa nchi kigeni jijini Kinshasa

Nairobi – Maafisa wa usalama wameimarisha usalama nje ya ubalozi wa nchi za Marekani, Uingereza na Ufaransa na Umoja wa Mataifa jijini Kinshasa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, kufuatia maandamano yaliyoanza kushuhudiwa wiki iliyopita na kulengwa kwa Magari yenye usajili wa kigeni, kulalamikia utovu wa usalama Mashariki mwa nchi hiyo.

Waandamanaji wanazituhumu nchi za Magharibi kwa kushindwa kuilaani Rwanda inayodaiwa kuwaunga mkono M23
Waandamanaji wanazituhumu nchi za Magharibi kwa kushindwa kuilaani Rwanda inayodaiwa kuwaunga mkono M23 REUTERS - ANGE KASONGO ADIHE
Matangazo ya kibiashara

Polisi hapo jana wametumia mabomu ya machozi, kuwasambaratisha waandamanaji waliokuwa wanaandamana kuelekea ubalozi wa Uingereza.

Vurugu zilishuhudiwa jijini Kinshasa wakati wa maandamano ya kulaani kuongezeka kwa utovu wa usalama mashariki mwa DRC.
Vurugu zilishuhudiwa jijini Kinshasa wakati wa maandamano ya kulaani kuongezeka kwa utovu wa usalama mashariki mwa DRC. REUTERS - STRINGER

Waandamanaji walivamia barabara kuu maarufu boulevard du 30 Juin, kwa lengo la kuzingira ubalozi wa Ufaransa, Marekani na ofisi za Monusco pamoja na balozi zanchi zingine za Magharibi, wakiamini kwamba nchi hizo zimeshindwa kuilaani nchi ya Rwanda inaodaiwa kuwaunga mkono waasi wa M23 mashariki mwa DRC.

‘‘Waende, tunataka waende watuwachie nchi yetu.’’ raia wa Kinshasa.

00:17

Sauti za waandamanaji jijini Kinshasa

 Waziri wa mambo ya ndani Peter Kazadi, amelaani vurugu hizo.

‘‘Tungependa kuwakumbusha kwamba makazi ya wanadiplomasia wa kigeni na wafanyakazi wa MONUSCO haziwezi kushambuliwa.’’ alisema Peter Kazadi, waziri wa mambo ya ndani.

00:26

Peter Kazadi, Waziri wa mambo ya ndani wa DRC

Kama hatua ya tahadhari, shule za kigeni katika mji mkuu zimefungwa tangu asubuhi ya leo, pamoja na maduka mengi katikati mwa jiji la Kinshasa.

Freddy Tendilonge, Kinshasa rfi Kiswahili.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.